Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Hawza, Ayatollah Makarem Shirazi katika maandiko yake alizungumzia suala la "Nafasi ya Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran katika maendeleo ya Fiqhi na Kanuni" katika Mnasaba wa kumbukumbu ya Ushindi wa Mapinduzi ya Kiislamu.
Muhtasari wa maandiko ya Ayatollah Makarem:
Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran yaliyoanzishwa chini ya Uongozi wa Imam Khomeini (r.a) na kupata ushindi, yaliifanya jamii kukabiliana na masuala mapya.
Utawala wa jamii kwa Mwanasheria mwenye ujuzi na msingi wa sheria za Kiislamu ulitoa jukwaa ambalo lilisababisha kuibuka kwa masuala mapya. Kwa hivyo, mahitaji mapya yaliundwa ambayo Serikali ilipaswa kukabiliana nayo, sawa sawa iwe inataka au la. Kwa hiyo, Mafaqihi ilibidi wafikirie juu ya utangamano wa masuala haya na kanuni za Kiislamu. Kutatua masuala haya kulipelekea kustawi kwa Fiqhi na kugunduliwa kwa uwezo wake wa juu.
Mkusanyiko wa yote hayo ulisababisha Seminari (Hawza) na Fiqhi kuingia katika mada hizi katika miongo michache iliyopita, na hivyo uwanja wa Fiqhi na Kanuni za Fiqhi zikaweza kupanuka kwa kiasi kikubwa kulingana na mahitaji haya.
Your Comment